Manchester United wameripotiwa kuwasiliana na Bologna kuomba taarifa kuhusu mchezaji wa kimataifa wa Uswizi Dan Ndoye, ambaye anatarajiwa kumenyana na Italia kwenye EURO 2024 Jumamosi jioni.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa Gianluca Di Marzio na Sky Sport Italia, Manchester United wamefanya uchunguzi wa awali na Bologna na wameomba taarifa kuhusu ada inayowezekana ya uhamisho.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa.
Vigogo hao wa EPL bado hawajaanza mazungumzo yoyote rasmi kwa ajili ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23.

Wamiliki wa Manchester United INEOS wanasemekana kufahamu wasifu wa Ndoye tangu alipokuwa na Nice kwenye Ligue 1, ikizingatiwa kwamba wao na United sasa wako chini ya kundi moja la umiliki.
Ndoye amefurahia mwanzo mzuri wa EURO 2024. Yeye na Uswizi bado hawajashindwa kwenye dimba hilo na wamefuzu kwa hatua ya 16 katika nafasi ya pili katika Kundi A. Watamenyana na Italia Olympiastadion mjini Berlin Jumamosi saa moja usiku.


