Renato Veiga yuko JMedical, kituo cha matibabu cha Juventus, na kwa sasa anafanyiwa uchunguzi wa kimatibabu kabla ya uhamisho wake wa Januari kutoka Chelsea.

Beki huyo wa pembeni anahamia Allianz Stadium kwa mkataba wa mkopo wa moja kwa moja, hivyo atarejea Stamford Bridge majira ya kiangazi bila kujali kitakachotokea katika kipindi cha miezi sita ijayo.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa.
Juventus watalipa ada ya €5m kumleta mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21 kwa mkopo kwa muda uliosalia wa msimu wa 2024-25, lakini Chelsea wanatarajiwa kuendelea kugharamia mshahara wa mchezaji huyo, ambao utasaidia kupunguza gharama kwa Bianconeri.


