WAKALI WAKUCHEKA NA NYAVU YANGA

Katika suala la kucheka na nyavu ndani ya Ligi Kuu Tanzania Bara ambayo ni ligi namba nne kwa ubora Afrika, Yanga hawana utani wakiwa ni namba moja kwenye eneo hili kwa kukusanya mabao mengi zaidi.

WAKALI WAKUCHEKA NA NYAVU YANGA

Baada ya mechi 22 ambazo ni dakika 1,980 safu ya ushambuliaji ya Yanga ni namba moja ikiwa imetupia jumla ya mabao 58 ikiwa na wastani wakufunga bao moja kila baada ya dakika 34.

Timu hiyo ilianza kwa mwendo wa kusuasua mzunguko wa kwanza ambapo mchezo wake wa kwanza ikiwa ugenini Agosti 29 2024 dhidi ya Kagera Sugar baada ya dakika 90 ubao ulisoma Kagera Sugar 0-2 Young Africans na mchezo wa pili ilikuwa Ken Gold 0-1 Yanga.

Katika dakika 180 safu ya ushambuliaji ya Yanga ilitupia mabao matatu huku ukuta ukiwa haujaruhusu bao ndani ya mechi hizo za ugenini ambapo bao la ushindi kwenye mchezo dhidi ya Ken Gold, Uwanja wa Sokoine, Mbeya lilifungwa na Ibrahim Bacca ambaye ni beki namba moja kwa kutupia mabao mengi ambayo ni manne.

Ukitazama chati ya utupiaji ndani ya kikosi cha Young Africans kinachonolewa na Miloud Hamdi kuna mastaa wawili ambao kila mmoja katupia mabao 10 kibindoni ndani ya Ligi Kuu Bara.

Prince Dube huyu ni nyota wa kwanza kufunga hat trick na Clement Mzize ni mzawa namba moja mwenye mabao mengi ndani ya ligi namba nne kwa ubora Afrika. Hapa ndipo ambapo upepo ulibadilika baada ya Dube kufungua ukurasa wa mabao ilikuwa ni Desemba 19 2024, Uwanja wa KMC, Complex.

WAKALI WAKUCHEKA NA NYAVU YANGA

Huu ulikuwa ni mchezo wa kwanza kwa Yanga kucheza KMC Complex ambapo awali walikuwa wanatumia Uwanja wa Azam Complex, baada ya dakika 90 ubao ulisoma Yanga 3-2 Mashujaa ya Kigoma, baada ya hapo ushindi wa Young Africans ikawa ni kuanzia mabao mawili kuendelea.

Maxi Nzengeli huyu ni nyota wa kwanza kufunga ndani ya kikosi cha Young Africans msimu wa 2024/25 ilikuwa dhidi ya Kagera Sugar, kibindoni ana mabao matano na katoa pasi 7 za mabao.

Yanga inaongoza ligi ikiwa na pointi 58 baada ya mechi 22 safu yao ya ushambuliaji ni namba moja kwa kufunga mabao mengi ambayo ni 58. Timun amba mbili ni Simba ambayo safu yao ya ushambuliaji imetupia mabao 52 baada ya mechi 21.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.