SIMBA IMEPIGWA BAO HAPA NA YANGA

Kwenye vita ya kuwania ubingwa ndani ya ligi kuu bara inayodhaminiwa na NBC ngoma bado ni mbichi huku Simba ikipigwa bao mazima na Yanga kwenye eneo la kucheka na nyavu.

SIMBA IMEPIGWA BAO HAPA NA YANGA

Kikosi cha Yanga kinachonolewa na Kocha Mkuu, Miloud Hamdi ni namba moja kwenye timu zenye mabao mengi ambayo ni 58 baada ya mechi 22 ambazo ni dakika 1,980 ikiwa na wastani wakufunga bao moja kila baada ya dakika 34.

Wakati Yanga ikiwa ni namba moja imewapiga bao watani zao wa jadi Simba kwenye eneo hilo kwa kuwaacha kwa tofauti ya mabao sita kwa kuwa safu ya ushambuliaji ya Simba imetupia jumla ya mabao 52.

Kikosi cha Simba kinachonolewa na Kocha Mkuu, Fadlu Davids inafuatiwa kimetupia mabao 52 baada ya kucheza mechi 21 ambazo ni dakika 1,890 msimu wa 2024/25 kikiwa na wastani wakutupia bao moja kila baada ya dakika 36.

Mnyama kwa msimu wa 2024/25 imekuwa na wastani wakufunga bao kwenye kila mchezo ambapo katika mechi 21 ambazo ilicheza ni mchezo mmoja pekee ilikwama kufunga ilikuwa dhidi ya Yanga.

SIMBA IMEPIGWA BAO HAPA NA YANGA

Katika mchezo huo wa mzunguko wa kwanza wa Kariakoo Dabi baada ya dakika 90 ubao wa Uwanja wa Mkapa ulisoma Simba 0-1 Yanga, bao la Kelvin Kijili ambaye alijifunga kwenye harakati za kuokoa hatari ndani ya uwanja.

Mchezo ambao Mnyama ilikusanya mabao mengi ilikuwa dhidi ya Dodoma Jiji ambao ulichezwa Uwanja wa KMC Complex kwenye mchezo huu baada ya dakika 90 ubao ulisoma Simba 6-0 Dodoma Jiji huku Kibu Dennis akifungua akaunti ya mabao baada ya kupitisha wiki 70 bila kufunga ndani ya ligi.

Jean Ahoua kwenye mchezo huo uliochezwa Machi 14 2024 alitupia mabao mawili akifikisha mabao 12 na pasi zake ni sita akiwa ni namba moja kwa wakali wenye mabao mengi ndani ya ligi.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.