Meneja wa Al-Sadd na mchezaji wa zamani wa Barcelona, Xavi Hernández Creus amesema anataka kurejea nyumbani Camp Nou na kuthibitisha maongezi yanaendelea baina ya vilabu hivyo viwili.

Klabu ya Al-Sadd ilitoa taarifa ambayo iliweka wazi kutaka kumbakiza meneja huyo lakini Xavi ameweka wazi matamanio yake ya kurejea nyumbani katika klabu yake ya zamani.
“Nimekuwa nikiongea na Barcelona kwa muda, tumemalizana,” alisema Xavi baada ya sare ya 3-3 dhidi ya Al-Duhail siku ya Jumatano, “Lakini yote yanategemeana na maongezi baina ya vilabu, wanahitaji kufikia makubaliano. Barcelona wamekuja kuongea, wote tuna hamu na msisimuko, tutaona kama litaenda kufanikiwa.
“Kiukweli nataka kurejea nyumbani. Natumaini itafanikiwa. Nina mkataba na sasa vilabu vinahitaji kukubaliana. Tayari wanajua nafasi yangu.” aliongeza.
Mkwanja umetema ndani ya kasino za meridianbettz, Mchezo maridhawa wa Aurora Beast Hunter unakupa nafasi sawa ya ushindi leo hii, kila mzunguko una nafasi ya kuibuka mshindi, na mkwanja wako unaupata kila mzunguko utakapo kamilika.


