Simba Queens Yavuna Mil 400

Timu ya wanawake  Simba Queens kutoka Tanzania imeweka rekodi ya kuwa timu ya kwanza kwa wanawake kufuzu hatua ya Nusu Fainal ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika baada ya kuitungua Green Buffaloes kwa mabao 2-0.

 

Simba Queens Yavuna Mil 400

Mchezo huo ulipigwa katika uwanja wa Grand Stade De Marrakech majira ya saa 4:00 usiku huku mchezo huo ulikuwa muhimu sana kwa Simba Queens kupata matokeo hayo ili waweze kuvuka hatua inayofuata.

Kutinga kwa nusu fainali kwenye Ligi ya Mabingwa Simba watapata Milioni 400 za Kitanzania kutokana na kufuzu hatua hiyo, huku Opa Clement akichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo.

Simba Queens Yavuna Mil 400

Mabao hayo mawili yalitupiwa kimyani na Asha Djafar katika dakika 64 na baadae Opa Clement akapachika bao la pili ambalo liliifanya Simba iongoze mpaka dakika 90 za mchezo kumalizika.

Timu hiyo ilianza safari yao kwa kupoteza mchezo wa kwanza kwa bao 1-0 dhidi ya mwenyeji Far Rabat, na mechi ya pili akashinda kwa mbao 2-0 dhidi ya Determine Girls ya Liberia na mechi ya jana ya kufuzu akashinda mabao mawili tena.

Simba Queens Yavuna Mil 400

Kocha Mkuu wa Simba Queens Charles Lukula  na Vijana wake sasa wanasubiria watapangwa na nani katika hatua hiyo ya nusu fainali huku wakiendelea kujiandaa na kujiweka vyema kwa mchezo huo unaofuata.


aviator

Ulishawahi kuwaza kuwa rubani wa maisha yako!! Kuwa rubani wa mchezo pendwa wa Aviator wa kasino mtandaoni. Aviator bonanza inazidi kutoa michongo ya mkwanja kwenye nyumba ya mabingwa. Unarusha ndege yako na unashinda, kuwa rubani wa kujivunia kwa kuibuka na mkwanja leo.

BONYEZA HAPA

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.