Ruvu Shooting Yamtangaza Kocha Mpya

Klabu ya Ruvu Shooting imemtambulisha Mbwana Makata kuwa Kocha wao mkuu atakayeinoa timu hiyo akirithi mikoba ya aliyekuwa kocha wa timu hiyo Charles  Boniphace Mkwasa.

 

Ruvu Shooting Yamtangaza Kocha Mpya

Makata amechukua nafasi hiyo ya Mkwasa ambaye amejiuzulu kuifundisha Ruvu Shooting baada ya kuwa na mwendelezo mbaya wa matokeo kwenye Ligi kuu ya NBC Tanzania Bara.

Kabla ya kutangazwa kuwa kocha wa timu hiyo, Mbwana Makata alishawahi kuinoa timu ya Dodoma jiji ambayo alipanda nayo Ligi huku akileta ushindani mkubwa kwenye ligi kabla ya kuanza kupata matokeo mabovu yaliyomfanya aondoke klabuni hapo.

Ruvu Shooting Yamtangaza Kocha Mpya

Lakini pia kocha huyo hakuishia kuifundisha Dodoma Jiji peke yake alipita klabu ya Mbeya Kwanza ambayo ilishuka daraja msimu jana baada ya kushindwa kupata matokeo yanayoridhisha.

Makata anaikuta timu hiyo katika nafasi ya 15 kwenye msimamo ikiwa na pointi zake 11 mpaka sasa.

Ruvu Shooting Yamtangaza Kocha Mpya

 

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.