Ismael Bennacer anajidhihirisha kuwa hawezi haiondolowi kwenye klabu ya Milan iliyopo chini ya Stefano Pioli huku ikijiandaa kwa duru mpya ya mazungumzo ya mkataba na wakala wake.

Kiungo huyo wa kati wa Algeria mwenye umri wa miaka 25 alikuwa kiungo muhimu katika ushindi wa Rossoneri wa 2-1 dhidi ya Salernitana, akikamilisha pasi 49, akishinda taboli tatu na kurejesha mipira 13.
Yeye ni nguvu kuu ya ubunifu katika kikosi, na ni mchezaji anaejua kulazimisha na kusaidia kimya kimya katika mchezo wa kujenga.

Kama ilivyoripotiwa na La Gazzetta dello Sport, Milan hawataki kumpoteza Bennacer katika miezi ijayo na wanataka kumsainisha mkataba mpya, huku mkataba wake wa sasa ukitarajiwa kuisha Juni 2024. Watakutana na wakala wake Enzo Raiola baadaye mwezi huu kujaribu kufikia makubaliano.
Klabu hiyo ilikutana na Raiola mwezi uliopita, ambapo walitoa ofa ya kitita cha euro milioni 3.8 kwa msimu pamoja na nyongeza, lakini ikawa wazi kwamba wangehitaji kuongeza idadi kidogo, huku Mualgeria huyo akitarajia mshahara wa Jumla ya €4.5m ikijumuisha nyongeza.
![]()

