Arteta Aitaja Arsenal Kucheza Nusu Fainali ya Champions League Ni Heshima Kubwa

Kocha wa Mikel Arteta amesema ni “heshima kubwa” kwa Arsenal kucheza nusu fainali ya UEFA Champions League kwa msimu wa pili mfululizo, huku akisisitiza kuwa timu yake iko tayari kutumia nafasi hiyo vizuri dhidi ya Atletico Madrid.

Arteta Aitaja Arsenal Kucheza Nusu Fainali ya Champions League Ni Heshima KubwaArsenal walifika nusu fainali kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2009 msimu uliopita, lakini walitolewa na mabingwa wa baadaye Paris Saint-Germain. Msimu huu, Arteta ana matumaini ya kuifikisha klabu hiyo fainali ya pili katika historia ya mashindano hayo makubwa barani Ulaya.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Licha ya kushuka kidogo kwa kasi yao katika Ligi Kuu England baada ya kupunguzwa kwa uongozi wao hadi pointi tatu na Manchester City, Arsenal walipata hamasa mpya baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya Newcastle United.

Arteta Aitaja Arsenal Kucheza Nusu Fainali ya Champions League Ni Heshima KubwaAkizungumza kabla ya mchezo wa kwanza utakaopigwa Madrid, Arteta alisema “Ulikuwa ushindi mkubwa dhidi ya Newcastle. Unaweza kuhisi mara moja nishati na kujiamini kuingia kwenye mchezo huu. Ni heshima kubwa kuwa hapa tena kwa mwaka wa pili mfululizo katika nusu fainali ya Champions League.”

Arteta Aitaja Arsenal Kucheza Nusu Fainali ya Champions League Ni Heshima KubwaArsenal, ambao walishinda Atletico 4-0 katika mchezo wa awali wa hatua ya makundi London, bado wanabaki timu pekee ambayo haijapoteza mechi katika mashindano ya msimu huu wa Champions League.

Arteta Aitaja Arsenal Kucheza Nusu Fainali ya Champions League Ni Heshima KubwaArteta alisema“Tunafahamu ugumu wa mchezo, lakini tumekuwa thabiti sana Ulaya. Lazima tucheze kwa kujiamini na hamasa kubwa ili tushinde.”

Arteta Aitaja Arsenal Kucheza Nusu Fainali ya Champions League Ni Heshima KubwaAliongeza kuwa uzoefu wa msimu uliopita hautakuwa sehemu ya mazungumzo ya moja kwa moja na wachezaji wake.“Hapana, si ujumbe mzuri sana kuzungumzia hilo. Tumejifunza, lakini mchezo wa kesho ni tofauti kabisa, hasa tukiwa ugenini,” alihitimisha.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.