Kocha wa Mikel Arteta amesema ni “heshima kubwa” kwa Arsenal kucheza nusu fainali ya UEFA Champions League kwa msimu wa pili mfululizo, huku akisisitiza kuwa timu yake iko tayari kutumia nafasi hiyo vizuri dhidi ya Atletico Madrid.
Arsenal walifika nusu fainali kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2009 msimu uliopita, lakini walitolewa na mabingwa wa baadaye Paris Saint-Germain. Msimu huu, Arteta ana matumaini ya kuifikisha klabu hiyo fainali ya pili katika historia ya mashindano hayo makubwa barani Ulaya.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Licha ya kushuka kidogo kwa kasi yao katika Ligi Kuu England baada ya kupunguzwa kwa uongozi wao hadi pointi tatu na Manchester City, Arsenal walipata hamasa mpya baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya Newcastle United.
Akizungumza kabla ya mchezo wa kwanza utakaopigwa Madrid, Arteta alisema “Ulikuwa ushindi mkubwa dhidi ya Newcastle. Unaweza kuhisi mara moja nishati na kujiamini kuingia kwenye mchezo huu. Ni heshima kubwa kuwa hapa tena kwa mwaka wa pili mfululizo katika nusu fainali ya Champions League.”
Arsenal, ambao walishinda Atletico 4-0 katika mchezo wa awali wa hatua ya makundi London, bado wanabaki timu pekee ambayo haijapoteza mechi katika mashindano ya msimu huu wa Champions League.
Arteta alisema“Tunafahamu ugumu wa mchezo, lakini tumekuwa thabiti sana Ulaya. Lazima tucheze kwa kujiamini na hamasa kubwa ili tushinde.”
Aliongeza kuwa uzoefu wa msimu uliopita hautakuwa sehemu ya mazungumzo ya moja kwa moja na wachezaji wake.“Hapana, si ujumbe mzuri sana kuzungumzia hilo. Tumejifunza, lakini mchezo wa kesho ni tofauti kabisa, hasa tukiwa ugenini,” alihitimisha.

