Kocha wa klabu ya Liverpool Jurgen Klopp ameonesha kufurahishwa na wachezaji wapya ambao wameingia kikosini katika dirisha hili kubwa la majira ya joto.
Jurgen Klopp amefanikiwa kukamilisha saini za wachezaji wawili katika eneo la kiungo la klabu hiyo ambao ni Alexis Macallister aliyotoka Brighton na Dominik Szoboszlai kutoka klabu ya RB Leipzig na kumpa furaha kocha huyo.
Kocha huyo amezungumzia wachezaji wake hao wapya akionesha ni mwenye furaha huku akisaema Macallister anacheza mpira mzuri kama ilivyokua kwa Dominik Szoboszlai hivo klabu hiyo inatarajia makubwa kutoka kwa nyota hao.
Kocha huyo tayari ameirudisha timu kambini rasmi kwajili ya maandalizi ya msimu ujao na wachezaji kadhaa wameshafanikiwa kujiunga na timu hiyo katika kambi ikiwemo wachezaji wake nyota kama Mohamed Salah na beki Alxender Arnold.
Liverpool chini ya kocha Jurgen Klopp imedhamiria kurudi kwa nguvu kubwa kuelekea msimu ujao, Kwani msimu uliomalizika hawakua vizuri mpaka kupelekea kukosa ushiriki wa michuano ya ligi ya mabingwa ulaya msimu uliopita.

