Vyanzo vingi vya habari vinadai David De Gea amekubali masharti binafsi na Fiorentina kama wakala huru na kandarasi ya mwaka mmoja pamoja na chaguo la kuongeza, kwa hivyo atalazimika kufanyiwa uchunguzi wa kimatibabu hivi karibuni.

Kipa huyo amekuwa nje ya soka kwa zaidi ya mwaka mmoja, tangu mkataba wake na Manchester United uliporuhusiwa kumalizika Julai 2023, kwani hakuweza kupata mradi ambao ulimsisimua.
Pia meridianbet inatoa michezo ya kasino ya mtandaoni kama vile, Aviator, poker, Roullette, sloti na mingine kibao. Ingia meridianbet na ucheze sasa.
Sasa amerejea na kujaribu tukio jipya katika Serie A, ametimiza miaka 34 ya kuzaliwa kwake.

Kulingana na mtaalam wa uhamisho wa Sportitalia Alfredo Pedullà, huu utakuwa mkataba wa mwaka mmoja wenye thamani ya €1m kwa msimu pamoja na bonasi.
Pia kuna chaguo la kuongeza kwa mwaka wa pili, ambapo mshahara wake utaongezwa mara mbili hadi €2m.
De Gea anatarajiwa kusafiri kwa ndege hadi Florence kufanyiwa uchunguzi wa kiafya ndani ya saa 48 zijazo, huku Viola wakianza msimu wao baadaye mwezi huu.


