AISHI MANULA KUREJEA AZAM NI ASILIMIA 100

Kipa wa Simba SC, Aishi Manula inaelezwa kuwa yupo kwenye rada za mabosi wa Azam FC ambao wanahitaji saini yake.

AISHI MANULA KUREJEA AZAM NI ASILIMIA 100

Ipo wazi kwamba Manula kwa msimu wa 2024/25 hajawa chaguo la kwanza ndani ya kikosi hicho kinachonolewa na Kocha Mkuu,Fadlu Davids.

Katika mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara hajaanza langoni mchezo hata mmoja na kwenye anga la kimataifa pia jina lake lilikuwa linaondolewa kwenye siku za safari.

Kwenye mechi zote za fainali ugenini na Tanzania, dhidi ya RS Berkane ni Moussa Camara, kipa namba moja wa Simba SC alianza na benchi alikuwa Ally Salim.

Taarifa zinaeleza kuwa mabosi wa Azam FC wanahitaji saini ya kipa huyo ambaye ni miongoni mwa wazawa wenye uwezo mkubwa awapo langoni.

AISHI MANULA KUREJEA AZAM NI ASILIMIA 100

Ikumbukwe kwamba wakati wa dirisha dogo Azam FC walituma maombi kwa Simba SC kuhitaji huduma ya Manula ila mabosi wa Simba SC wakabainisha kuwa bado wanahitaji huduma yake.

Julai 2022, Air Manula aliongeza mkataba na Simba SC ambao unatarajiwa kugota mwisho msimu wa 2024/25 ukifika tamati.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.