Kocha wa SL Benfica, Jose Mourinho, anajiandaa kwa mchezo mkubwa wa mchujo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Real Madrid, katika mechi inayobeba hisia kali kwake binafsi. Huku jina lake likitawala vichwa vya habari kabla ya pambano hilo, tetesi zimekuwa zikiongezeka kuhusu uwezekano wa kurejea Santiago Bernabeu.
Mourinho aliinoa Real Madrid kati ya mwaka 2010 hadi 2013, akivunja utawala wa Barcelona kwa kutwaa taji la La Liga kwa alama 100, rekodi iliyotikisa Hispania wakati huo. Urithi wake Madrid umebaki kuwa wa mafanikio makubwa yaliyochanganyika na ushindani mkali wa hali ya juu.
Kutokana na uvumi kuwa rais wa klabu hiyo, Florentino Perez, huenda anatafuta kocha mwenye uzoefu wa ushindi ili kuiongoza timu katika kipindi cha mpito, Mourinho aliulizwa moja kwa moja kuhusu uwezekano wa kurejea. Kwa kawaida yake ya uwazi, alikiri kuwa bado ana hisia maalum kwa klabu hiyo.
“Nilitoa kila kitu kwa Real Madrid. Nilifanya mazuri na mabaya, lakini nilitoa kila nilichokuwa nacho,” alisema. “Niliondoka miaka 12 iliyopita, lakini bado ninapokutana na mashabiki wa Madrid popote duniani, kuna hisia ileile, kwamba nilitoa kila kitu kwa klabu.”
Uvumi huo pia umechangiwa na taarifa kuwa Mourinho ana kipengele maalum katika mkataba wake na Benfica kinachorahisisha kuvunja mkataba. Hata hivyo, aliweka wazi kuwa kipengele hicho kililenga kulinda maadili wakati wa kipindi cha uchaguzi wa klabu, ili kutoa uhuru kwa pande zote iwapo kungekuwa na mabadiliko ya uongozi.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa




