Trabzonspor Kumsajili Onana Huku United Wakitaka £43M Dirisha Kubwa la Usajili

André Onana alihamia kwa mkopo katika klabu ya Trabzonspor mwaka jana, lakini anatarajiwa kurejea katika klabu ya Manchester United mwishoni mwa msimu.

Trabzonspor Kumsajili Onana Huku United Wakitaka £43M Dirisha Kubwa la Usajili

Onana amekuwa akicheza mara kwa mara kwa Trabzonspor msimu huu. Hata hivyo, Manchester United wamearifiwa kuwa klabu hiyo ya Ligi Kuu ya Uturuki haiko tayari kulipa kati ya £40 milioni hadi £43 milioni ili kumsajili kipa huyo majira ya kiangazi, kwa mujibu wa ripoti ya MEN.

Onana alijiunga na Trabzonspor kwa mkopo mwezi Septemba baada ya kushuka katika chaguo la makipa ndani ya Manchester United kufuatia ujio wa kipa wa Ubelgiji Senne Lammens.

Lammens sasa amejiimarisha kama kipa namba moja katika uwanja wa Old Trafford baada ya kuonyesha kiwango kizuri katika mechi kadhaa alizocheza kwa klabu hiyo.

Manchester United walitarajia Onana angeonyesha kiwango kizuri akiwa Trabzonspor ili klabu hiyo ya Uturuki iwe tayari kumsajili moja kwa moja, kwani timu hiyo ya Premier League inataka kurejesha sehemu ya ada ya takribani £43.8 milioni waliyoilipa Inter Milan mwaka 2023 kumsajili kipa huyo wa Cameroon.

Ingawa Mlinda Mlango huyo ameanza mechi 20 za ligi kwa Trabzonspor wanaoshika nafasi ya tatu, kipa huyo mwenye umri wa miaka 29 amekuwa akikosa uthabiti wa kiwango akiwa chini ya kocha Fatih Tekke.

Kutokana na hali hiyo, Manchester United wamejulishwa kuwa Trabzonspor hawako tayari kuongeza muda wa golikipa huyo kubaki klabuni hapo baada ya msimu kumalizika.

Trabzonspor Kumsajili Onana Huku United Wakitaka £43M Dirisha Kubwa la Usajili

Makamu wa rais wa Trabzonspor Zeyyat Kafkas alieleza, “Kwa kuwa kiwango cha fedha kinachotakiwa na Manchester United kwa ajili ya kumnunua André Onana kiko kati ya euro milioni 45 hadi 50, rais wetu ameeleza ukweli huo kwa uwazi kulingana na uwezo wa Trabzonspor.”

Aliongeza kuwa taarifa hiyo haijaathiri mawazo ya Onana, kwani kipa huyo anatamani kuendelea kucheza Ulaya iwapo hatarudi England.

Kocha Tekke pia amesema golikipa huyo ndiye atakayeamua hatma yake: “Onana yuko hapa kwa mkopo. Kuna mechi ambazo hakufanya vizuri, lakini pia kuna nyingi ambazo alifanya vizuri. Nimeridhishwa sana na mtazamo wake, si kwa kiwango tu bali pia tabia yake.”

Ingawa inaonekana anaweza kuondoka majira ya kiangazi, Andres ana nia ya kupigania nafasi ya kuwa kipa namba moja katika Manchester United atakaporejea Manchester baadaye mwaka huu.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.