Carrick Hana Haraka Kujua Mustakabali wake Manchester United

Kocha wa muda wa Manchester United, Michael Carrick, amesema anafurahia kuinoa klabu hiyo lakini hana haraka ya kupata majibu kuhusu hatma yake, huku timu hiyo ikikaribia kufuzu michuano ya UEFA Champions League.

Carrick Hana Haraka Kujua Mustakabali wake Manchester UnitedCarrick, aliyewahi kuwa kiungo wa United, aliteuliwa kushika nafasi ya ukocha hadi mwisho wa msimu baada ya kuondoka kwa Rúben Amorim mwezi Januari kufuatia mzozo wa ndani ya klabu.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Tangu achukue jukumu hilo, Carrick ameiongoza timu hiyo kupata ushindi muhimu dhidi ya Manchester City na Arsenal, matokeo yaliyoisogeza United hadi nafasi ya tatu katika msimamo wa Premier League.

Carrick Hana Haraka Kujua Mustakabali wake Manchester United“Nimesema mara nyingi, ninafurahia kuwa hapa na ninaipenda nafasi niliyonayo,” alisema Carrick Alhamisi kuelekea mchezo wa Jumatatu dhidi ya Brentford.

“Tumeanza kupata matokeo mazuri na bado tuna nafasi ya kuboresha zaidi. Kuna mambo mengi bado tunahitaji kufikia,” aliongeza, akisisitiza kuwa timu inaendelea kujijenga hatua kwa hatua.

Carrick Hana Haraka Kujua Mustakabali wake Manchester UnitedKuhusu mustakabali wake, Carrick alisema hana presha ya kutaka majibu ya haraka. “Kwa kweli sihisi kama ninahitaji kufuatilia muda maalum. Mambo yatakuwa wazi wakati sahihi utakapofika,” alihitimisha kocha huyo wa zamani wa timu ya taifa ya England.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.