De Ligt Atamfuata De Jong Barcelona

Nyota wa Ajax ambaye ni nahodha wa klabu hii Matthijs de Ligt amepania uhamisho wa kwenda Barcelona mwisho wa msimu, atamfuata De Jong!

Nyota huyu kinda anachukuliwa kama mmoja wa walinzi bora zaidi duniani akiwa na miaka 19 tu. Staa huyu anatajwa kuwepo kwenye rada ya Barcelona na baadhi ya klabu zingine kubwa duniani.

Barcelona ambao tayari wamekamilisha usajili wa mchezaji mwenzie na De Light, Frenkie de Jong atakayetimkia kwenye soka la Hispania msimu ujao wa Joto bila shaka wanahitaji kumvuta na huyu mlinzi bora ambaye bado ni kinda kabisa.

Kwa mujibu wa Mundo Deportivo, De Ligt anataka kumfuata De Jong pale Camp Nou msimu huu unapoisha. Barcelona watahitaji kulipa, paundi milioni 65 na nyongeza ya paundi milioni 9 ili kumsainisha kinda huyu.

Juventus walikuwa wanahusishwa na nyota huyu, kwa mujibu wa Tuttorsport siku kadhaa zilizopita Juventus walikuwa wanamatumaini kwa watashinda mbio za kumnasa kinda huyu kutoka Ajax.

Klabu nyingine inayoungana na Barcelona na Juventus kwenye mbio hizi ni Manchester City. Kama De Light anapendelea zaidi kujiunga na Barcelona basi Juve na Man City tayari wana nafasi finyu zaidi, wataweza kumpata kama Barcelona wakishindwa kumchukua.

3 Komentara

    Habar njema

    Jibu

    Iko vizuri.

    Jibu

    Iko vizuri

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.