Tyson Fury ameweka wazi kuwa pambano analolitaka zaidi kwa sasa ni dhidi ya mpinzani wake mkubwa Anthony Joshua, lakini mambo si rahisi kama inavyoonekana. Kabla ya yote, Fury anatakiwa kurejea ulingoni wikendi hii dhidi ya Arslanbek Makhmudov mjini London.

Licha ya mipango ya awali ya pambano kati yake na Joshua msimu huu wa joto, hali ilibadilika baada ya AJ kupata ajali ya gari mwezi Desemba. Hali hiyo imemlazimu Joshua kufikiria pambano la maandalizi kwanza kabla ya kuingia kwenye vita kubwa kama ya Fury.
Hata hivyo, Fury hana muda wa kusubiri sana. Ameweka wazi kuwa Joshua ndiye mpinzani anayemtaka mara moja baada ya pambano lake lijalo, akiamini kuwa AJ anapaswa kuwa tayari kuingia ulingoni bila kuchelewesha mazungumzo zaidi.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Kwa upande mwingine, timu ya Joshua inaonekana kuwa na mpango tofauti kidogo. Promota Eddie Hearn amesisitiza kuwa AJ anahitaji pambano la kujipima kwanza kutokana na hali yake ya kimwili baada ya ajali, na jina linalotajwa zaidi kama maandalizi ni Deontay Wilder, ambaye amerejea kwenye kiwango kizuri hivi karibuni.

Iwapo mipango hii itafanikiwa, mashabiki wa ndondi wanaweza kushuhudia ratiba ya moto, Joshua dhidi ya Wilder, kisha pambano kubwa la kihistoria kati ya Fury na Joshua mwishoni mwa mwaka. Hilo ndilo pambano ambalo dunia imekuwa ikilisubiri kwa muda mrefu sana.


