Klabu ya Brighton ambayo inaongozwa na kocha mkuu Graham Potter itakuwa nyumbani hapo kesho kuwaalika Leicester City baada ya kupoteza mchezo uliopita dhidi ya Fulham kwa mabao 2-1.

Brighton katika mechi tano za ligi kuu walizocheza wameshinda wameshinda michezo mitatu, sare moja na wamepoteza mchezo mmoja, wakati kwa upande wa Leicester ni timu ambayo ambayo haijashinda hata mechi moja ikiungana na Everton, pamoja na Wolveshampton hizi timu toka ligi ilipoanza hawajashinda mchezo wowote zaid ya kupoteza na kupata sare.
Brighton imefanya sajili ya wachezaji mbalimbali kama vile Billy Gilmour, Pervis Estupinan, Levi Colwil na wengine wengi ambao wataenda kuimarisha timu hiyo katika msimu huu ambapo wameanza vizuri , Lakini pia wamemuuza mchezaji wao ambaye alikuwa na mchango kwenye timu yao.

Wanaenda kukutana na Leicester City ambayo msimu huu imeuza wachezaji muhimu kwenye kikosi cha kwanza lakini wakashindwa kutafuta mbadala wa wachezaji hao na hatimaye kuanza vibaya msimu na mpaka sasa ndio wanaoshikilia mkia kwenye msimamo wa Epl.

