Kocha mkuu wa FC Barcelona, Hansi Flick, amesema timu yake haitabadilisha mtindo wake wa kucheza licha ya kukutana na Newcastle United katika mchezo wa hatua ya 16 bora ya UEFA Champions League.

Barcelona wanatarajiwa kucheza ugenini katika Uwanja wa St James’ Park leo Jumanne katika mchezo wa mkondo wa kwanza wa hatua hiyo, huku wakitajwa kuwa na nafasi kubwa ya kufuzu robo fainali kutokana na ubora wa kikosi chao na nafasi yao ya juu katika ligi ya Hispania.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Hata hivyo, Flick ameonya kuwa Newcastle ni timu hatari licha ya kushika nafasi ya 12 katika Premier League, akisisitiza kuwa nguvu ya kifedha na ushindani mkubwa wa ligi hiyo huifanya kuwa mojawapo ya ligi bora zaidi duniani.

Akizungumza na waandishi wa Habari hapo jana, Flick alisema kuwa ligi ya England ina timu nyingi imara na ndio sababu timu sita kutoka ligi hiyo zimefanikiwa kufika hatua ya 16 bora ya Champions League msimu huu.
Kocha huyo aliongeza kuwa Barcelona wataendelea kushikilia falsafa yao ya kucheza soka la kushambulia na kumiliki mpira, akisema wanataka kucheza kwa mtindo wao wa kawaida ili kuwafanya mashabiki wao wajivunie timu hiyo.

Flick pia alikiri kuwa Newcastle wana wachezaji wenye kasi kubwa na uwezo wa kushambulia kwa kushtukiza, hivyo Barcelona wanapaswa kuwa makini wanapokutana katika mchezo huo muhimu wa kuwania kufuzu hatua inayofuata ya mashindano hayo.

