HIVI NDIVYO SIMBA ILIVYOTINGA NUSU FAINALI KIBABE

Kikosi cha Simba chini ya Kocha Mkuu, Fadlu Davids, Aprili 9 2025 kiliandika rekodi ya kutinga hatua ya nusu fainali Kombe la Shirikisho Afrika kwa ushindi wa penati 4-1 baada ya dakika 90 za pili ubao wa Uwanja wa Mkapa kusoma Simba 2-0 Al Masry.

HIVI NDIVYO SIMBA ILIVYOTINGA NUSU FAINALI KIBABE

Fadlu kabla ya mchezo aliweka wazi kuwa mpango mkubwa ni kupata ushindi na kuzuia kutofungwa ndani ya dakika 90 jambo ambalo wachezaji walitimiza kwa ushirikiano ndani ya dakika 90, safu ya ulinzi chini ya Hamza Jr ilifanya kazi kubwa kwa ushirikiano na Zimbwe Jr ambaye ni nahodha, Shomari Kapombe Legend wa muda wote Simba.

Katika dakika 45 za mwanzo Simba waliwanyanyua mashabiki wao kupitia kwa Ellie Mpanzu dakika ya 22 na Steven Mukwala dakika ya 32 na ikumbukwe kwamba kwenye mchezo wa robo fainali ya kwanza Uwanja wa Suez Canala ulisoma Al Masry 2-0 Simba hivyo mshindi alitafutwa kwa penati.

Mukwala alipachika bao la pili kwa pigo la kichwa akitumia krosi iliyotoka kwenye mguu wa beki wakupanda na kushuka Mohamed Hussein Zimbwe Jr ambaye alikuwa kwenye majukumu yake kama Camara ambaye alifanya kazi yake kuzuia mpira usiguse nyavu za Simba.

HIVI NDIVYO SIMBA ILIVYOTINGA NUSU FAINALI KIBABE

Kwa upande wa Simba mpigaji wa kwanza wa penati alikuwa ni Jean Ahoua, penati ya pili mpigaji alikuwa ni Steven Mukwala, penati ya tatu mpigaji alikuwa ni Kibu Dennis na penati ya nne ya maamuzi ilipigwa na Shomari Kapombe, wapigaji wote wa Simba walifunga kwa kutumia mguu wakulia, huku Moussa Camara kipa wa Simba akiokoa penati mbili kati ya tatu ambazo walipiga Al Masry.

Mlinda mlango wa Al Masry, Gad hakuwa na bahati kwenye mchezo huo kwa kuwa wapigaji wa Simba walifunga penati zote walizopiga huku Camara akiokoa mbili na moja ilizama mazima nyavuni.

Simba inatinga hatua ya nusu fainali na mchezo ujao wa hatua hiyo unatarajiwa kuchezwa Uwanja wa Mkapa itakuwa dhidi ya Stellenbosch FC ya Afrika Kusini Aprili 20 na kete ya pili itamaliziwa ugenini Aprili 27, Afrika Kusini.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.