Klabu ya Inter Milan imethibitisha kuwa itamkosa nahodha wake na mfungaji kinara, Lautaro Martinez, katika mchezo wa Jumapili wa Serie A dhidi ya Como baada ya kupata majeraha ya misuli ya mguu.
Kupitia taarifa rasmi, Inter ilieleza kuwa “Vipimo vya kitabibu vilivyofanyika leo (Ijumaa) vimeonesha kuwa ana mshtuko mdogo wa misuli kwenye ndama ya mguu wa kushoto,” huku wakiongeza kuwa hali yake “itafanyiwa tathmini upya katika siku zijazo.”
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Ripoti kutoka vyombo vya habari vya Italia zinaashiria kuwa mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 28 anaweza kurejea mapema wiki ijayo wakati Inter watakapocheza nyumbani dhidi ya Cagliari. Hii inatoa matumaini kwa mashabiki wa Inter ambao wanategemea mchango wake mkubwa safu ya ushambuliaji.
Kwa sasa Inter wanaongoza msimamo wa ligi kwa tofauti ya pointi saba dhidi ya mabingwa watetezi, Napoli, huku zikiwa zimesalia mechi saba pekee kumalizika kwa msimu. Hata hivyo, ushindani bado ni mkali huku AC Milan wakishika nafasi ya tatu kwa tofauti ya pointi tisa.
Martinez, ambaye anaongoza orodha ya wafungaji akiwa na mabao 16 msimu huu, aliwahi kukaa nje kwa wiki sita kati ya Februari na Machi kutokana na majeraha ya misuli. Alirejea wikiendi iliyopita na kufunga mabao mawili katika ushindi wa 5-2 dhidi ya AS Roma.
Kutokana na kukosekana kwake, kocha wa Inter, Cristian Chivu, anatarajiwa kuwaanzisha Marcus Thuram na Pio Esposito katika safu ya ushambuliaji. Inter wanakabiliwa na mtihani mgumu ugenini dhidi ya Como, wakilazimika kushinda ili kuendelea kulinda nafasi yao kileleni mwa ligi

