Klabu ya Raja Casablaka ya Morocco, inayosimamiwa na kocha wa zamani wa klabu ya Simba SC Fadlu Davids, imegoma kuendelea kucheza mechi zake za Ligi Kuu ya Botola Pro hadi timu nyingine zinazoshiriki ligi hiyo ziweze kumaliza michezo yao ya viporo.

Hadi sasa, Raja Casablanca wamecheza mechi 15, huku washindani wao wenye viporo wakiwa Wydad Casablanca, RS Berkane, FAR Rabat, na Olympic de Safi, ambao wote wamecheza mechi 12 kila mmoja. Hatua hii imechukuliwa na Raja kwa lengo la kusawazisha mechi zao za kimataifa na kuhakikisha usawa kwenye msimamo wa ligi.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Kocha mkuu wa Raja casablanca Fadlu David amesema kuwa ni haki kwa timu zote kucheza idadi sawa ya mechi ili kushindana kwa usawa na kuongeza ushindani mkali kwenye ligi, huku mashabiki wakitarajia uamuzi huu usuluhishwe haraka ili ligi iendelee bila vikwazo.

