Ligi kuu ya NBC Tanzania hapo jana iliendelea kwa michezo kadhaa ambapo mchezo wa usiku saa 3:00 ulikuwa ni kati ya bingwa mtetezi Yanga vs KMC kule Azam complex ambapo wananchi waliweza kuibuka na ushindi.

Bao hilo la ushindi lilifungwa mapema kabisa dakika ya 4 na Maxi Nzengeli huku mechi hiyo ikiwa ni kushambulia na kulinda.
Yanga walicheza kikubwa sana kwani kuanzia dakika ya kwanza mpaka ya mwisho walikuwa wanalishambulia lango la KMC ambao wanadhaminiwa na Meridianbet lakini vijana hao wa Moalin walikaa imara.
Mashabiki wengi wa Young Africans walidhani itakuwa ni mechi nyepesi sana kwao kwani mechi ya mwisho walivyokutana katika dimba hilo KMC walipoteza kwa idadi kubwa ya mabao lakini jana ni bao moja pekee.


