Timu ya Al Ahly imetwaa taji la Klabu Bingwa kwa mara ya 11 hapo jana baada ya kutoka sare ya 1-1 dhidi ya timu ya Wydad Casablanca kwenye fainali ya pili.

Wydad ambaye alikuwa ni bingwa mtetezi msimu uliopita, ameshindwa kutetea taji hilo baada ya mechi ya mkondo wa kwanza kupoteza kwa mabao 2-1 na hivyo kufanya aggregate kuwa (3-2).
Wydad alilipata taji hilo kutoka kwa Ahly msimu uliopita kwa kumfunga mabao 2-0 na sasa amelipoteza mbele ya huyo huyo Mbabe wa Afrika ambaye ana mataji 11 hadi sasa barani Afrika.

Klabu hiyo Misri inakauwa klabu ya kwanza mabayo ina mataji mengi zaidi Afrika akifuatiwa na Zamalek ya Misri pamoja na TP Mazembe ya Congo ambao wote wana mataji 05 kila mmoja.
Baada ya kubeba ubingwa huo, Ahly ambao ndio mabingwa watapewa Dola Milioni 4 (T.sh Bilioni 9.4) wakati Wydad atapewa Dola Miolioni Milioni 2 (T.sh Bilioni 4.7)

