Azam na Yanga Kuzichapa Kesho, Mzizima Derby

Ligi kuu ya NBC kuendelea kesho ambapo ni Mzizima Derby inayowakutanisha kati ya Azam FC na Yanga ambao ni mabingwa watetezi wa ligi msimu uliopita.

 

Azam na Yanga Kuzichapa Kesho, Mzizima Derby

Azam FC wapo nafasi ya tatu hadi sasa baada ya kucheza michezo yao 17, wamepata ushindi mara 11, sare nne na wamepoteza michezo miwili, alama zao 37 kibindoni hadi sasa.

Wakati Yanga wao wapo kileleni kwenye msimamo wakiwa wamejishindia mechi zao 14 kati ya 17, sare mbili na kupoteza mchezo mmoja tuu, wakiwa na alama 44 tofauti pointi 6 na anayeshikilia nafasi ya pili.

Azam na Yanga Kuzichapa Kesho, Mzizima Derby

Kaimu Afisa habari wa Azam Hasheem Ibwe amesema kuwa pointi zao tatu zitanzia kesho kwenye mechi yao itakayopigwa katika Uwanja wa Mkapa majira saa 2:15 usiku baada ya kupata sare mbili mfululizo.

Mechi ya kwanza kukutana msimu huu kwenye ligi timu zilitoshana nguvu kwa kutoa sare ya 2-2 huku Yanga akiwa ndiye anasawazisha mabao yote baada ya vijana wa Kally Ongala kutangulia kufunga.

 

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.