Simba Kucheza Mchezo wa Kukamilisha Ratiba Leo

Klabu ya Simba inatarajia kucheza mchezo wao wa kukamilisha ratiba ya michuano ya Mapinduzi leo baada ya kuvuliwa ubingwa kwenye mchezo wake wa kwanza kwa kuchapwa bao 1-0.

 

Simba Kucheza Mchezo wa Kukamilisha Ratiba Leo

Simba ilichapwa bao hilo katika kipindi cha pili dakika ya 75 na timu ya Mlandege FC na kushindwa kusawazisha bao hilo mpaka mpira kumalizika na kuwafanya washikilie mkia kwenye kundi.

Mlandege ndiye kinara wa kundi hilo akiwa na alama 4 baada ya kutoa sare mchezo wao wa kwanza na kuja kujipatia pointi kwa Mnyama dakika za jioni za mchezo huku Wekundu hao wakiwaweka wachezaji wao ambao mara nyingi huwa hawaanzi.

Leo hii ni mchezo wa kukamilisha ratiba kwani kwenye kila kundi inapita timu moja, hivyo hata Simba akishinda mechi hii ya leo bado atarejea nyumbani kutokana na kuwa mwenye pointi nyingi ndiye anayesonga mbele.

Simba Kucheza Mchezo wa Kukamilisha Ratiba Leo

Hapa inaangaliwa je Mnyama mwenye kocha wa Kibrazil watarudi Dar es salaam patupu? bila kushinda hata mchezo mmoja?. Mchezo wa leo watamenyaana dhidi ya KVZ.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.