Ligi kuu ya NBC Tanzania Bara kuendelea kesho kwa michezo mitatu ambapo kati ya hiyo michezo, mchezo wa mapema ni kati ya Singida Big Stars dhidi ya Geita Gold majira ya saa 10:00 Jioni.

Mchezo wa Singida utapigwa katika uwanja wa CCM Kirumba ambapo vijana hao wa Hans wakiwa wametoka kuchukua pointi tatu mchezo uliopita kwa Walima Zabibu kwa bao pekee la Gomes.
Kesho ni zamu ya Wachimba Dhahabu ambao wao wametoka kutoa sare ya pili mfululizo huku wakihitaji pointi tatu muhimu zitakazowawezesha kuwa kwenye nafasi nzuri kwenye msimamo wa ligi.
Singida wapo nafasi ya 4 baada ya kushinda mechi zao 10, sare 4, na kupoteza mara 4 wakiwa na pointi zao 34 huku ushindi wa hapo kesho utawafanya wafikishe pointi 37 zitakazowaweka kwenye nafasi ya 3.

Vijana wa Minziro wapo wapo nafasi ya 7 kwenye ligi,wakiwa wameshinda mechi zao 5, sare 9 na kupoteza mara 4, pointi 24 kibindoni. Tofauti yao ni pointi 10 hadi sasa. Nani kuibuka na pointi tatu zote kesho?

