Ancelotti Anaweza Kuiongoza Brazil Katika Mechi za Kufuzu WC June 2

Ripoti kutoka Hispania zinaonyesha kuwa Carlo Ancelotti huenda akawa kocha wa Brazil kwa ajili ya mechi za kufuzu Kombe la Dunia mwezi Juni, huku Real Madrid tayari wakiwa wamempanga Xabi Alonso kutoka Bayer Leverkusen kama mrithi wake.

Ancelotti Anaweza Kuiongoza Brazil Katika Mechi za Kufuzu WC June 2

Kocha huyo wa Kiitaliano haitarajiwi kuendelea kuwa kwenye benchi la Real Madrid baada ya msimu huu, lakini kuna uwezekano akaondoka hata kabla ya hapo.

Pia meridianbet inatoa michezo ya kasino ya mtandaoni kama vile, Aviator, poker, Roullette, sloti na mingine kibao. Ingia meridianbet na ucheze sasa.

Kuna tetesi kuwa Ancelotti anaweza kufutwa kazi iwapo atashindwa kuifunga Barcelona kwenye fainali ya Copa del Rey wikendi hii.

Wakati huo huo, Relevo wameripoti kuwa Real Madrid hawatamweka Ancelotti kwa ajili ya kampeni ya Kombe la Dunia la Klabu litakalofanyika Marekani kuanzia Juni hadi Julai.

Ancelotti Anaweza Kuiongoza Brazil Katika Mechi za Kufuzu WC June 2

Iwapo ataondoka mapema kiasi hicho, basi Muitaliano huyo atakuwa huru kuiongoza Brazil katika mechi muhimu za kufuzu Kombe la Dunia dhidi ya Ecuador tarehe 6 Juni na Paraguay tarehe 9 Juni.

Ingawa bado anahusishwa na vilabu vya Roma na Milan, inaonekana tayari ameshafanya uamuzi wa kuifundisha timu ya taifa ya Brazil, maarufu kama Selecao.

Kwa upande wa Real Madrid, tayari wamepata mbadala wake, kwani leo Mkurugenzi Mtendaji wa Bayer Leverkusen, Fernando Carro, amethibitisha kuwepo kwa “makubaliano ya kiungwana” yatakayomruhusu Xabi Alonso kuondoka iwapo klabu aliyowahi kuichezea itahitaji huduma yake.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.