Arsenal wamewatangulia wapinzani wao wa London Chelsea katika mbio za kumnasa kiungo wa Brighton Moises Caicedo.
Caicedo mwenye miaka 21, anatarajiwa kuwa moto katika dirisha la usajili la majira ya kiangazi baada ya kuisaidia Seagulls kupata kufuzu kwa Uropa kwa msimu ujao.
Nyota huyo wa Ligi ya Uingereza amekuwa katikati ya chumba cha injini cha Roberto De Zerbi lakini bosi huyo wa Italia amejiuzulu kwa kumpoteza raia huyo wa Ecuador.
The Gunners walikuwa wanapanga kumnunua kinda huyo Januari mwaka jana lakini hawakuweza kukamilisha makubaliano kabla ya Caicedo kusaini mkataba mpya utakaodumu hadi 2027.
Football Insider wanaripoti Chelsea pia wanamwinda kiungo huyo wa kati lakini itabidi washindane na wakuu wa Emirates ambao wako tayari kuvunja kibubu ili kuimarisha kikosi cha Mikel Arteta.
Washika mitutu hao wa London Kaskazini waliripotiwa kuweka mezani dau la pauni milioni 70 kwa ajili ya mchezaji huyo wa kimataifa mwenye mechi 30 katika dirisha la majira ya baridi, ingawa hilo lilikataliwa haraka kwani Brighton walikuwa na nia ya kumaliza kampeni kwa nguvu kamili.
Lakini sasa upande wa Pwani ya Kusini wanasemekana kuwa tayari kusikiliza matoleo yanayolingana na alama sawa na hawatasimama katika njia ya Caicedo kama anataka kusonga mbele.
The Blues ya Todd Boehly ingependa kumleta Muamerika huyo Kusini Stamford Bridge lakini matumizi yao ya kupita kiasi katika mwaka jana yanafanya wasiweze kuingia katika vita vya kuwania zabuni na The Gunners.