Arthur Melo ameorodhesha baadhi ya sababu zilizomfanya ajiunge na Fiorentina kwa mkataba wa mkopo wa msimu mzima kutoka Juventus katika mahojiano ya hivi karibuni na Sport Mediaset.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 alirejea Turin msimu huu wa joto kufuatia kipindi kibaya alichotumia kwa mkopo na Liverpool mnamo 2022-23, wakati huo alilazimika kucheza kwa dakika 13 tu kwa kikosi cha kwanza cha Jurgen Klopp.
Odds kubwa kasino ya mtandaoni na michezo ya sloti ni vitu vinavyoweza kubadilisha maisha yako kwa kukupatia pesa nyingi. Ingia mchezoni hapa.
Sasa, kiungo huyo wa zamani wa Barcelona yuko mbioni kuanza upya chini ya Vincenzo Italiano huko Tuscany na anahisi kama tayari ametulia.

“Ninapenda sana hapa, tayari nilijua baadhi ya wachezaji kwenye timu. Ni rahisi kufikia mahali ikiwa tayari unamfahamu mtu, najisikia vizuri sana na ninataka kujifunza, kuanza ubingwa mara moja.”
Arthur kisha akafichua kuwa Italiano ni moja ya sababu kuu zilizochangia uamuzi wake wa kusaini Fiorentina.
Hakuwa anamfahamu binafsi, lakini alikuwa ametazama mechi za timu yake na anapenda jinsi anavyocheza. Fiorentina walikuwa na msimu mzuri mwaka jana na fursa ilipopatikana ya kuja hapo alifurahi sana.

Tembelea duka la ubashiri-Meridianbet kutandika jamvi lako kwa odds kubwa.
Kisha kocha akampigia simu, baada ya kuongea naye alikuwa na uhakika wa 100% kuwa hapo ni mahali pazuri. Walizungumza mengi, alikuwa mzuri sana nami na sasa anaweza kujifunza mengi kutoka kwake.
Akiwa Liverpool msimu uliopita, Arthur aliumia sana kutokana na majeraha na masuala ya utimamu wa mwili na hadi mwisho wa muda wake Anfield alikuwa amecheza mechi nyingi zaidi kwa upande wa wachezaji wa akiba kuliko kikosi cha kwanza.
“Jeraha nililopata nikiwa Juventus kisha Liverpool lilifanya mambo kuwa magumu kwangu. Ilikuwa pigo kubwa. Lakini hii ni soka, inaweza kutokea. Nilijifunza mengi, nilikuwa na wakati wa kufanya kazi na kukua. Sasa natazama mambo mazuri yaliyo mbele yetu”.

Ukiwa na meridianbet odds kubwa, kasino ya mtandaoni na michezo ya sloti.
Sasa nataka kufanya mambo vizuri. Nilitaka sana kuja hapa, ilikuwa nzuri kwamba klabu ilifanya kila kitu kunifikisha huko. Sasa, nataka kuwa na msimu mzuri. Nataka kushinda na kujifunza kisha tutaona kitakachotokea. Alimaliza hivyo mchezaji huyo.

