AS Roma wamekuwa washindi wa kwanza wa Ligi ya Europa Conference baada ya kuifunga Feyenoord 1-0 na kuhakikisha Jose Mourinho bado hajafungwa katika fainali kubwa za Ulaya.
Klabu hiyo kutoka mji mkuu wa Italia iliishinda Feyenoord 1-0 katika fainali ya kwanza kabisa ya Ligi ya Conference mjini Tirana, Albania, huku Nicolo Zaniolo akifunga bao pekee katika mchezo huo katika kipindi cha kwanza.

Baada ya mchezo huo kuanza kwa kishindo, huku kukiwa na changamoto nyingi kutoka kwa pande zote mbili, Feyenoord walifanikiwa kumiliki mpira kwa kiasi kikubwa.
Hata hivyo, Feyernood walishinda kubadilisha umiliki huo kuwa magoli na kuruhusu AS Roma kutangulia katika dakika ya 32 kwa goli safi la Nicolo Zaniolo ambalo lilidumu mpaka dakika ya 90.
Meneja wa AS Roma, Jose Mourinho, ambaye ameshinda Ligi ya Mabingwa, Ligi ya Europa na Kombe la Uefa, ndiye meneja wa kwanza kushinda mataji yote makubwa ya Uefa kwa ngazi ya vilabu.
Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.


