Gwiji wa Argentina na Serie A, Gabriel Omar Batistuta, amesema kuwa hajaona tofauti yoyote kati ya Lautaro Martinez na Julian Alvarez, na anaamini kuwa wanaweza kucheza pamoja katika timu ya taifa ya Argentina, lakini “mmoja wao atapaswa kujitoa zaidi kwa ajili ya mwenzake.”

Batistuta, aliyewahi kung’ara Fiorentina, Roma na Inter, alimpongeza nahodha wa Inter, Lautaro Martinez, na kusema kuwa mzawa wake huyo ana uwezo mkubwa wa kushirikiana na Julian Alvarez kama washambuliaji wa kwanza katika timu ya taifa.
“Iwapenda wote,” Batistuta aliambia TyC Sports. “Ni tatizo zuri kwa Scaloni. Sijui ataamuaje.”
Wote wawili wanacheza vizuri, wanafunga mabao, wanapress, wanashika mpira na kupiga pasi. Sioni tofauti kati yao. Zaidi ya hapo, wote ni viongozi katika timu zao, na kila mmoja anaweza, kwa uwezo wake mwenyewe, kuiweka ngumu safu ya ulinzi ya wapinzani. Alisema Gwiji huyo.



