Batistuta: Hakuna Tofauti Kati ya Lautaro na Alvarez, Lakini Mmoja Lazima Ajitoe Kwaajili ya Argentina

Gwiji wa Argentina na Serie A, Gabriel Omar Batistuta, amesema kuwa hajaona tofauti yoyote kati ya Lautaro Martinez na Julian Alvarez, na anaamini kuwa wanaweza kucheza pamoja katika timu ya taifa ya Argentina, lakini “mmoja wao atapaswa kujitoa zaidi kwa ajili ya mwenzake.”

Batistuta: Hakuna Tofauti Kati ya Lautaro na Alvarez, Lakini Mmoja Lazima Ajitoe Kwaajili ya Argentina

Batistuta, aliyewahi kung’ara Fiorentina, Roma na Inter, alimpongeza nahodha wa Inter, Lautaro Martinez, na kusema kuwa mzawa wake huyo ana uwezo mkubwa wa kushirikiana na Julian Alvarez kama washambuliaji wa kwanza katika timu ya taifa.

“Iwapenda wote,” Batistuta aliambia TyC Sports. “Ni tatizo zuri kwa Scaloni. Sijui ataamuaje.”

Wote wawili wanacheza vizuri, wanafunga mabao, wanapress, wanashika mpira na kupiga pasi. Sioni tofauti kati yao. Zaidi ya hapo, wote ni viongozi katika timu zao, na kila mmoja anaweza, kwa uwezo wake mwenyewe, kuiweka ngumu safu ya ulinzi ya wapinzani. Alisema Gwiji huyo.

Batistuta: Hakuna Tofauti Kati ya Lautaro na Alvarez, Lakini Mmoja Lazima Ajitoe Kwaajili ya Argentina

Aliongeza kuwa, Lakini watahitaji kuombwa kufanya hivyo. Kutoka nje inaonekana inawezekana, lakini katika hali kama hizi, mmoja lazima ajitoe zaidi kwa mwenzake atoke kwenye sehemu yake ya faraja na acheze kwa ajili ya mwingine. Lakini kwa mtazamo wa nje, inaonekana wanaweza kucheza pamoja.

Katika mahojiano hayo hayo, Batistuta alisema mtindo wa uchezaji wa timu nyingi siku hizi unamchosha, na akaeleza kuwa washambuliaji wa aina aliyokuwa yeye au Bobo Vieri “hawapo tena” katika soka la kisasa.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.