Kocha mkuu wa Spurs Antonio Conte amerejea kufanya kazi na Tottenham baada ya kufanyiwa upasuaji wiki iliyopita ili kuondoa kibofu chake cha nyongo.

Spurs ilitangaza Jumatano iliyopita kwamba kocha huyo wa Italia alilazimika kuingia chini ya upasuaji baada ya kulalamika kupata maumivu makali ya tumbo yanayohusishwa na cholecystitis.
Conte alikosa ushindi wa 1-0 wa Tottenham katika Ligi Kuu ya Uingereza dhidi ya Manchester City wikendi iliyopita, huku msaidizi wake Cristian Stellini akiongoza kikosi hicho kupata ushindi.
Kocha huyo mwenye umri wa miaka 53 alisafiri kwa ndege kutoka Italia hadi Uingereza mapema wiki hii na kusimamia mazoezi siku ya leo kabla ya safari ya wikendi hii kuelekea Leicester.

Hata hivyo, bado haijathibitishwa na Tottenham iwapo Conte atakuwa dimbani kwenye Uwanja wa King Power siku ya Jumamosi.
Kulingana na Huduma ya Kitaifa ya Afya ya Uingereza, utaratibu aliofanyiwa Conte unaweza kuchukua takriban mwezi mmoja “kurejea kwenye shughuli zako za kawaida”.
Tottenham, ambayo iko katika nafasi ya tano kwenye Ligi ya Primia, itacheza mchezo wao dhidi ya Leicester halafu itaanza safari ya kwenda Milan kwa mechi ya mkondo wa kwanza wa hatua ya 16 bora ya Ligi ya Mabingwa Jumanne.

