Liverpool tayari wanaanza kutafuta mbadala wa Andy Robertson hata kabla beki huyo hajaondoka majira haya ya joto na pendekezo lao ni David Raum.

Nahodha wa RB Leipzig, David Raum, ameibuka kuwa mmoja wa malengo ya Liverpool, kulingana na ripoti ya TEAMtalk.
Robertson anatarajiwa kuondoka kwa mabingwa hao wa EPL mwishoni mwa msimu huu mkataba wake utakapomalizika. Taarifa rasmi ya klabu ilithibitisha kuwa baada ya misimu tisa yenye mafanikio makubwa katika Anfield, nahodha huyo wa Scotland ataondoka rasmi majira ya joto.
Inaelezwa kuwa Tottenham Hotspur wanaweza kumsajili Robertson kwa uhamisho wa bure, ingawa dili hilo litategemea kama Spurs watafanikiwa kubaki kwenye EPL.
Kwa upande mwingine, Liverpool wanamwona Raum kama mbadala anayefaa kutokana na uzoefu wake, lakini si wao pekee wanaomuhitaji. Manchester United pia wanatajwa kufuatilia beki huyo wa kushoto wa timu ya taifa ya Ujerumani, wakitaka kuongeza ushindani kwa Luke Shaw.


