Dier Aongeza Miaka 4 Spurs.


KIUNGO mkabaji wa Tottenham Hotspur, Eric Dier amerefusha mkataba wake kambini mwa miamba hao wa soka ya Uingereza hadi mwishoni mwa msimu wa 2024.

Dier, 26, aljiunga na Tottenham mnamo 2014 baada ya kuagana rasmi na kikosi cha Sporting Lisbon nchini Ureno kwa kima cha Sh560 milioni.

Dier aongeza Miaka 4 Spurs.

“Nafurahi sana kwamba nitakuwa sehemu ya kikosi kitakachotegemewa na Tottenham katika kipindi cha misimu kadhaa ijayo,” akatanguliza Dier ambaye pia ana uwezo wa kutamba akiwa beki wa kati.

Tottenham walinipa fursa ya kudhihirisha uwezo wangu uwanjani katika soka ya Uingereza. Wamenifanyia mengi ambayo natambua na kuthamini. Ni matarajio yangu kwamba nami nitaendelea kujitahidi na kuwatambisha katika kipindi hiki ninapovalia jezi zao,” akaongeza Dier.

Lengo langu ni kushirikiana vilivyo na kocha pamoja na wanasoka wengine ili kushindia Tottenham idadi kubwa zaidi ya mataji ya haiba kubwa. Ningependa kuondoka Tottenham nikifahamu kwamba nimefanya yote ambayo yamo ndani ya uwezo wangu katika juhudi za kuwavunia mataji muhimu ndani na nje ya kampeni za soka ya Uingereza,”.

-Dier

Hadi kufikia sasa, kiungo huyo amewajibishwa na Tottenham katika jumla ya mechi 239 na akapachika wavuni mabao 11.

Mnamo Julai 8, 2020, Dier alipigwa marufuku ya mechi nne na kutozwa faini ya Sh5.6 milioni kwa kosa la kumvamia shabiki aliyemtusi uwanjani mnamo Machi 2020.

Tukio hilo lilitokea mwishoni mwa mechi iliyoshuhudia Tottenham wakibanduliwa na Norwich City kwenye kipute cha kuwania ubingwa wa Kombe la FA msimu huu.

Dier aongeza Miaka 4 Spurs.

Erick pia alionywa na FA kwamba atakuwa katika hatari ya kuadhibiwa vikali zaidi katika siku za usoni iwapo atarudia makosa ya sampuli hiyo.

Tukio hilo lilifanyika mnamo Machi 4 wakati wa mechi ya raundi ya tano ya Kombe la FA iliyoshuhudia mshindi akiamuliwa kwa mikwaju ya penalti. Licha ya mchezaji huyo kupachika wavuni mkwaju wake, waajiri wake Tottenham walipoteza mechi hiyo na hatimaye kubanduliwa nje ya kipute cha Kombe la FA.

Wakati huo, kocha Jose Mourinho alikataa kabisa kuzungumzia suala hilo, akionya kwamba Tottenham na Dier wangalijipata katika hatari ya kuadhibiwa vikali zaidi iwapo yeye angefichua msimamo wake wa kutetea kikosi chake na matendo ya mwanasoka wake huyo.

Dier anajivunia kuvalia jezi za timu ya taifa ya Uingereza katika mechi 40 za hadi kufikia sasa.


Kwa sababu ya thamani ya pesa yako, kwa kila muamala unaofanya wa kuweka pesa kwenye akaunti yako ya Meridianbet unapata 5% bonasi.

Soma Zaidi

45 Komentara

    safi sana Dier piga kazi

    Jibu

    Safii sana#Meridianbettz

    Jibu

    Dier yuko vizuri namkubali sana

    Jibu

    Safi sana

    Jibu

    Safi sana#meridianbettz

    Jibu

    Spurs sio rahisi kumruhusu died kuondoka kwa sasa

    Jibu

    Safii hii inaonyesha kuwa uwongozi wa tottenham umekubali kazi yake na kumuongeza mkataba dier

    Jibu

    Spurs wapo vizuri na wamefanya vyema kumuongezea mkataba maana yupo vizuri

    Jibu

    Asante kwa nakala mana hapa inaonyesha jinsi gani mchezaji mwenye matamanio anavyo taka kufanya kitu kinzuri kwenye timu aliyopo kabla hajaondoka nampongeza sana Eric dier anaipenda timu yake anataka aweke historia kuwa alifanya kitu muhimu kwa Tottenham .iko tafauti sana na kwetu Tanzania mchezaji kabla hajaonyesha mafanikio kwenye klabu yake akipata kishawishi tu kwenye klabu nyingine anaaza sababu ambazo hazina mashiko wachezaji mnapaswa kuiga mafanikio sio kuiga ufahari. #meridianbettz

    Jibu

    Eric Dier anakibarua cha kumfanya Mourinho azidi kumuamini kwenye kikosi chake

    Jibu

    Erick yupo vizuri naona Tottenham wameamua kumuamini inabidi na yy kuonyesha kipaji chake

    Jibu

    Hongera sana dier

    Jibu

    Safii sana

    Jibu

    Pongez kwako dier piga kazi wakuamin Zaid uxiwaangushe

    Jibu

    Good news

    Jibu

    Inapendeza

    Jibu

    Makala nzur

    Jibu

    Habari njema

    Jibu

    habari nzuri sana

    Jibu

    Dier ni mchezaj mzuri

    Jibu

    Waoow Good news

    Jibu

    Ila kwa upande mwngne Eric dier alizingua sana kutokana na tukio ambalo alilolifanya mnamo julai 8 2020 amwaka huu kikwel n tukio la aibu sana kwa club ya Tottenham chin ya kiongoz kocha mkuu Jose Mourinho ila sio la kulizungumzia sana ila habar njema sana kwa bek huyu wa Kati kuongeza mkataba mwingine mpaka 2024 iko poa sana 👍 tunatumain alichokiongela kuhusu Hotspur miaka minne atafanya vzur kwan tunatambua uwezo wa huyu bek wa kati

    Jibu

    Vizurii

    Jibu

    Dier ni beki kisiki,anastaili kuendelea hapo spurs.

    Jibu

    habar njema

    Jibu

    Habari moto moto

    Jibu

    Habar njema

    Jibu

    Habali njema kwetu mashabiki

    Jibu

    Ni vizur

    Jibu

    Hongera zako#meridianbett

    Jibu

    Vzr

    Jibu

    Saafi sana

    Jibu

    Good 👍 news

    Jibu

    Safi sana

    Jibu

    Maoni:safi

    Jibu

    Hiyo ndo safi sana

    Jibu

    Dier amekua na humuimu kubwa sana pale Tottenham

    Jibu

    Habari nzuri

    Jibu

    Safi Sana kwa Tottenham kumuongezea mkataba dier Ni mchezaji mzuri sana #meridianbettz

    Jibu

    sidhani Kama spurs watakubali dier aondoke

    Jibu

    Ni vizuri

    Jibu

    Safiiii sana

    Jibu

    Inapendeza

    Jibu

    Good news 👍👍

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.