Kiungo wa kati wa Atalanta Ederson anasisitiza kuwa anafuraha sana na washindi hao wa Ligi ya Europa, lakini analengwa na Liverpool na ana hamu ya kuijua Ligi kuu.

Mbrazil huyo amekuwa mmoja wa watu muhimu katika kikosi cha Gian Piero Gasperini waliponyakua ushindi wa 3-0 dhidi ya Bayer Leverkusen kwenye Fainali ya Ligi ya Europa.
Pia walifika Fainali ya Coppa Italia dhidi ya Juventus na kupata nafasi ya nne kwenye Serie A kwa kufuzu kwa Ligi ya Mabingwa.
“Nina furaha sana nikiwa Atalanta. Nimeshinda taji kubwa, nimejumuishwa vyema. Mustakabali wangu ni jambo ambalo halinisumbui. Kinachonitia wasiwasi sasa hivi ni kufanya vizuri hapa na timu ya Brazil, na kuacha hisia chanya kwa sababu ni mara yangu ya kwanza kuitwa.” Alisema Ederson.

Amekuwa akihusishwa sana na uwezekano wa kuhamia Liverpool, ambao pia wameelekeza macho yao kwa mchezaji mwenzake wa Atalanta Teun Koopmeiners, ingawa Mholanzi huyo anaonekana kuwa karibu zaidi na Juventus badala yake.
Alipoulizwa kuhusu mustakabali wake, Ederson alikiri kwamba alikuwa tayari kuhamia Uingereza.
Sijui, nimeifikiria sana, napenda Italia, nimezoea, lakini nina hamu ya Ligi Kuu, kwa hivyo sijui. Bado ninakua, kwa hivyo sijui kama nitasalia Italia, nadhani bado nina zaidi ya kuthibitisha. Ikiwa nitaenda mahali pengine, basi pia. Nitaendelea kukua. Alisema mchezaji huyo.


