Terzic Aachana na Borussia Dortmund

Kocha Edin Terzic ambaye alikua kocha wa klabu ya Borussia Dortmund ametangaza kuachana na klabu hiyo baada ya kuitumikia klabu hiyo kwa takribani miaka miwili na mafanikio klabuni hapo.

Kocha Terzic huyo amesema anaona ni wakati sasa wa klabu ya Borussia Dortmund kuongozwa na mtu mwingine na yeye kwenda kutafuta changamoto nyingine nje ya klabu hiyo, Kwani amefanya kazi klabuni hapo kwa takribani miaka 10  na leo amemua kutimka ndani ya timu hiyo.terzic“Wapendwa Borussians, ingawa inaniuma sana sasa hivi, nataka kuwajulisha kuwa kuanzia leo, nitaondoka BVB. Ilikuwa heshima kubwa kuiongoza klabu hii kuu hadi kwenye ushindi wa DFB-Pokal na hivi karibuni kufika kwenye fainali ya Ligi ya Mabingwa.”

“Baada ya fainali yetu pale Wembley, niliomba mazungumzo na uongozi kwa sababu, baada ya miaka kumi BVB, ikiwemo miaka mitano katika timu ya ukocha na miaka miwili na nusu kama kocha mkuu, nahisi kwamba kuanzia sasa mwanzilishi mpya anapaswa kuongoza mchakato huu mpya.terzicKocha Terzic akiitumikia klabu hiyo kama kocha mkuu kwa misimu miwili amefanikiwa kubeba taji la DFB Pokal na kuifikisha klabu hiyo fainali ya ligi ya mabingwa ulaya msimu ulimalizika ambapo walipoteza kwa mabao mawili kwa bila mbele ya Real Madrid, Huku akiwa kocha wa kwanza kuipeleka Dortmund fainali ya ulaya baada ya miaka 10.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.