Kwa mujibu wa Tuttosport, klabu ya Ligi Kuu ya Uingereza, Nottingham Forest inamfuatilia kwa karibu kocha wa Torino Ivan Juric ambaye anaweza kuwa kocha anayefuata wa Serie A kuhamia Uingereza.

Mtaalamu huyo wa Croatia ana mkataba hadi 2024, lakini kulingana na Tuttosport hatma yake katika klabu hiyo haina uhakika ikizingatiwa kwamba hajafurahishwa na mikakati ya uhamisho ya Granata.
Gazeti hilo la mjini Turin limeripoti kuwa Nottingham Forest inamfikiria kocha huyo wa zamani wa Verona na Genoa kwa msimu ujao, ingawa sio klabu pekee ya Ligi Kuu ya Uingereza inayotaka kupata huduma yake.

Hata hivyo, Juric anasalia kuangazia Torino wakati msafara wake umeanza mazungumzo ya awali na baadhi ya vilabu vinavyovutiwa. Kocha huyo mwenye umri wa miaka 47 ameshinda mechi 21 kati ya 54 akiwa kocha wa Torino, sare 13 na kupoteza 20.
Juric alijiunga na Torino kutoka Verona msimu wa joto wa 2021, na kuiongoza Granata hadi nafasi ya kumi ikiwa na alama 50, 13 zaidi ya ilivyokuwa katika kampeni iliyopita, huku Nottinh ham wakiwa bado na hali mbaya ambapo wapo nafasi ya 20.


