Kikosi cha Yanga kilichosafiri hapo jana kuelekea Tunisia kwaajili ya mchezo wao wa marudiano wa Kombe la Shirikisho barani Africa dhidi ya Club Africain kimewasili hii leo kujiandaa na mchezo ambao utapigwa siku ya Jumatano.

Yanga ilipitia Dubai kwanza kabla ya kwenda Tunisia moja kwa moja huku wakiwa na matumaini ya kupata matokeo dhidi ya Club Africain ili waweze kusonga mbele kwenye hatua ya makundi.
Kwenye mechi hii ya marudiano hakuna sare, hapa inabidi timu mojawapo ishinde na na nyingine itoke, hivyo Young Africans kama wanahitaji kusonga mbele kwenye michuano hii wanahitaji zaidi kupata magoli kuanzia mawili au hata moja na wasiruhusu bao.

Club Africain wao walimtoa Kipanga kwa kumbamiza mabao 7-0 wakiwa nyumbani kwao na sasa wakafanikiwa kupata sare ugenini hivyo Yanga wanakibaru kizito cha kufanya huko Tunisia.

Ulishawahi kuwaza kuwa rubani wa maisha yako!! Kuwa rubani wa mchezo pendwa wa Aviator wa kasino mtandaoni. Aviator bonanza inazidi kutoa michongo ya mkwanja kwenye nyumba ya mabingwa. Unarusha ndege yako na unashinda, kuwa rubani wa kujivunia kwa kuibuka na mkwanja leo.
BONYEZA HAPA

