Christian Pulisic anakiri kuwa amekuwa akipitia kipindi kigumu akiwa na AC Milan pamoja na timu ya Taiaf ya Marekani , lakini anaamini mpira utagonga goti lake na kuingia wavuni, na mambo yatabadilika.

Mshambuliaji huyo alikuwa kwenye kiwango cha kushangaza mwaka 2025, lakini hajafanikiwa kufunga bao lolote kwa AC Milan katika mwaka huu wa kalenda, jambo linaloongeza ukame wake wa kimataifa unaoendelea tangu 2024.
Alipata tena usiku mgumu wakati Marekani walipokuwa wakijiandaa kwa jukumu lao la kuwa wenyeji wa FIFA World Cup 2026 majira ya joto, ambapo walipoteza nyumbani kwa mabao 5-2 dhidi ya Ubelgiji.
“Kwangu mimi inakatisha tamaa. Ninahisi ningeweza kufanya vizuri zaidi kwenye moja ya nafasi. Niliikosa, halafu wao wakaenda kufunga, na mchezo ukabadilika. Inanikera sana, bila shaka.” Christian Pulisic aliwaambia waandishi wa habari.
Nafasi hiyo ilikuwa pale alipoupiga mpira juu ya lango wakati matokeo yalikuwa 1-1, na muda mfupi baadaye Ubelgiji wakachukua uongozi wa 2-1.
Sasa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 anajaribu kubaki na mtazamo chanya licha ya changamoto anazokutana nazo mbele ya lango, akiwa na AC Milan pamoja na timu ya Marekani.


