Mkurugenzi wa Como, Carlalberto Ludi, amesema kuna uwezekano mkubwa kwamba Nico Paz ataendelea mwaka mwingine klabu, na pia ana uhakika kuhusu kukaa kwa Cesc Fabregas hadi jambo la ajabu litokee.

Kipaji cha Argentina, Nico Paz, amekuwa miongoni mwa wachezaji bora wa Serie A msimu huu, jambo lililosababisha vyombo kadhaa vya habari kudai kwamba Real Madrid wangemrudisha mwishoni mwa msimu.
Hata hivyo, katika mahojiano na Radio Lo Sport, mkurugenzi wa michezo wa Como, Ludi, alisema ana uhakika kwamba Paz ataendelea msimu mwingine kwenye Stadio Sinigaglia.
Kuna uwezekano mkubwa kwamba Nico Paz ataendelea kuwa nasi kwa mwaka mwingine,” Ludi alisema kupitia Calciomercato.com.
Kama ilivyotajwa hapo awali na Rais wa Como, Mirwan Suwarso, uamuzi kuhusu mustakabali wa Nico Paz uko kabisa mikononi mwa Real Madrid, kwani Merengues wana chaguo la kumrudisha M Argentina huyo hadi 2027 na wanaweza kulinganisha ofa yoyote ambayo Como inaweza kupokea katika kipindi hicho.
“Hadithi daima ni ile ile. Hatuwezi kudhibiti mapenzi ya wengine. Tuna furaha naye na yeye pia ana furaha sana kuwa nasi. Mashindano yoyote ya Ulaya yangetutengenezea faida. Uwezekano wa kukaa kwake bado ni mkubwa leo, hata kama Kombe la Dunia pia linapaswa kuzingatiwa.” Ludi akaendelea.

Como wanashikilia nafasi ya nne katika msiammo wa Serie A wakiwa na alama tatu mbele ya Juventus na Roma, hivyo hata kocha wa Azzurri, Cesc Fabregas, amekuwa akihusishwa na uvumi.

