UEFA Imethibitisha Fiorentina Inaweza Kuipa Italia Nafasi 9 Michuano ya Ulaya

UEFA imethibitisha kwamba ikiwa Fiorentina itashinda Konferensi Ligi na kumaliza nje ya timu saba za juu, kutakuwa na timu tisa za Italia barani Ulaya msimu ujao.

UEFA Imethibitisha Fiorentina Inaweza Kuipa Italia Nafasi 9 Michuano ya Ulaya

Kulikuwa na mkanganyiko wa kweli juu ya hali ya uchezaji, kwani mambo yalitikiswa na Italia kupata nafasi ya ziada ya Ligi ya Mabingwa kutokana na kuwa kileleni mwa viwango vya mashindano ya vilabu.

Pia meridianbet inatoa michezo ya kasino ya mtandaoni kama vile, Aviator, poker, Roullette, sloti na mingine kibao. Ingia meridianbet na ucheze sasa.

Ikiwa Fiorentina watashinda Fainali dhidi ya Olympiacos mnamo Mei 29, basi watafuzu moja kwa moja kwa Ligi ya Europa.

Mkurugenzi wa UEFA Giorgio Marchetti aliiambia Sky Sport Italia jana kwamba ikiwa Viola watanyanyua kombe na kumaliza katika nafasi ya nane kwenye Serie A, basi nafasi ya kufuzu kwenye Ligi ya Konferensi itachukuliwa na timu iliyo nafasi ya tisa badala yake.

UEFA Imethibitisha Fiorentina Inaweza Kuipa Italia Nafasi 9 Michuano ya Ulaya

Hiyo itakuwa aidha Torino au Napoli, kwenda katika raundi ya mwisho ya kampeni.

Inamaanisha kuwa timu tisa za juu katika Serie A zote zitafuzu kwa mashindano ya UEFA, kwani tano bora au sita, kulingana na Atalanta huingia Ligi ya Mabingwa, ya sita, saba na Fiorentina ikiingia kwenye Ligi ya Europa, kisha ya tisa Konferensi ligi.

 

Acha ujumbe