Mchezaji aliyepambwa zaidi na Real Madrid Karim Benzema ataondoka katika klabu hiyo baada ya miaka 14.

Mshambuliaji huyo wa Ufaransa Benzema mwenye miaka 35, alishinda mataji 25 wakati alipokuwa Madrid na kufunga mabao 353 katika mechi 647 na kuwa mfungaji bora wa pili wa muda wote wa Real baada ya Cristiano Ronaldo.
Taarifa ya klabu imesema; “Real Madrid na nahodha wetu Karim Benzema wamekubali kumaliza kipindi chake kizuri na kisichosahaulika kama mchezaji wa klabu yetu. Klabu ingependa kuonyesha shukrani na mapenzi kwa mchezaji ambaye tayari ni mmoja wa magwiji wetu wakubwa.”
Kazi ya Karim Benzema katika Real Madrid imekuwa mfano mzuri wa tabia na taaluma, na amewakilisha maadili ya klabu yetu. Karim Benzema amepata haki ya kuamua mustakabali wake.

Madridistas na mashabiki wote duniani wamefurahia soka yake ya ajabu na ya kipekee, ambayo imemfanya kuwa mmoja wa icons kubwa wa klabu yetu na mmoja wa hadithi kubwa za soka duniani.
“Real Madrid ni nyumbani kwake na daima itakuwa nyumbani kwake, na tunamtakia yeye na familia yake kila la heri katika hatua hii mpya ya maisha yake.”
Benzema, Mchezaji Bora wa sasa wa Ballon d’Or na UEFA, alijiunga na Real kutoka Lyon Julai 2009 kwa ada ya uhamisho ya euro milioni 35.

Anashika nafasi ya tano kwenye orodha ya wachezaji waliocheza Real mara nyingi zaidi na kunyakua mataji yake nchini Uhispania ni pamoja na Ligi ya Mabingwa tano, Kombe la Dunia la Klabu tano, Kombe la Super Cup mara nne, mataji manne ya LaLiga, matatu ya Copas del Rey na manne ya Super Cups ya Uhispania.
Benzema amekuwa akihusishwa na kuhamia klabu ya Al-Ittihad ya Saudi Arabia.

Real wamethibitisha kuwa watafanya “tendo la kitaasisi la kumuenzi na kumuaga” Benzema katika mji mkuu wa Uhispania siku ya Jumanne mbele ya rais wa klabu Florentino Perez.

