Real Madrid wamewalenga wapinzani wao Barcelona kufuatia madai ya Joan Laporta kuwa ni klabu ya utawala kutokana na video ambayo imetembea mtandaoni.

Rais wa Barcelona Laporta alijitetea kwa utetezi wa klabu yake katika mkutano na waandishi wa habari hapo jana huku kukiwa na madai kuwa walifanya malipo kwa Jose Maria Enriquez Negreira, makamu wa rais wa zamani wa kamati ya kiufundi ya waamuzi.
Blaugrana wanakabiliwa na uchunguzi wa UEFA huku waendesha mashtaka nchini Uhispania wakifuatilia mashtaka kwa madai ya ufisadi. Barca wanatuhumiwa kulipa zaidi ya Euro milioni 7 kwa kampuni inayomilikiwa na Negreira.
Laporta aliamua kuangazia Madrid alipodai kuwa klabu yake haina kesi ya kujibu, akipendekeza Real “kihistoria na kwa sasa” wamependelewa na maamuzi ya usuluhishi, akihusisha na dikteta wa zamani wa Uhispania Francisco Franco.

Hilo lilipelekea Los Blancos kujibu kwa video ya ajabu na ndefu ambayo ilitangazwa kwenye mitandao ya kijamii na Real Madrid TV, ikielezea viungo vya Barcelona na Franco.
Hapo awali video iliuliza ni timu gani ya serikali? “kwa kujibu wazi maoni ya Laporta kabla ya kuandaa kesi yake. Camp Nou ilizinduliwa na waziri mkuu wa Franco, Jose Solis Ruiz,” video hiyo ilisema.
Barcelona ilimfanya Franco kuwa mwanachama wa heshima mnamo 1965 …ilimkabidhi tuzo mara tatu.

Video hiyo pia ilionyesha mafanikio ya Barcelona kwa kulinganisha na Madrid wakati wa enzi ya Franco ya kwanza, 1939 hadi kifo chake mnamo 1975, pamoja na kwamba uongozi wake ulisaidia kuiokoa klabu hiyo kutokana na kufilisika mara tatu.

