Mara baada ya kusaini mkataba wa mwaka mmoja wa nyongeza, mlinzi wa klabu ya soka ya Montpellier mwenye umri wa miaka 42, Vitorino Hilton amefunguka na kusema kuwa ana sababu zake za kudumu katika soka namna hiyo.
Mshindi huyo mara mbili wa Ligue 1 Conforama aliiambia RMC: “Unatakiwa kufanya mazoezi kila siku. Ninajiandaa katika njia maalum kiasi kwamba huwa ninasahau umri wangu wa sasa. Ninauweka pembeni kabisa. Wakati mwingine ninasahau kabisa kama nina umri wa miaka 42 na ninacheza na mtu kama Joris Chotard ambaye ana umri wa miaka 18. Ninadhani kwamba jambo hilo linanisaidia sana kujisikia fiti na kujitoa hasa uwanjani.
βMiaka minne iliyopita nilidhani ya kwamba mke wangu atanisihi niache kucheza soka.β
βMiaka minne ama mitano iliyopita mke wangu aliniambia niache kucheza soka kwa muda huo. Kwa sasa yupo hapa pembeni yangu akinipa sapoti kubwa sana na ananiambia kuwa nisichoke, niendelee. Inanipa moyo sana na nguvu zaidi. Upendo wangu kwenye soka bado upo moyoni mwangu. Ninaipenda soka tangu nikiwa mtoto mdogo kabisa. Na ninadhani kuwa nitaendelea kuipenda soka hivi hivi na nina ari kubwa ya kucheza mpira wa miguu.β
Kwa sasa Hilton ameongeza muda wa miezi 12 mbele wakati ambapo Souleymane Camara, mwenzake wa klabu moja waliyoipa mafanikio na kutwaa taji mwaka 2012 wakiwa na Montpellier, yupo anakula bata zake kwenye boti akiwa na umri wa miaka 37 tu!
βNinapenda sana kucheza!β
Hilton anasema kuwa: Nilikuwa na kocha nikiongea naye ambapo tulizungumza sana na kisha nikaongea na Mkurugenzi wa Michezo, Bruno Carotti. Nilimpa mawazo yangu ya kupenda kuendelea kucheza soka. Wiki moja mbele Rais ainitumia ujumbe akinitaka nirudi klabuni. Tulizungumza kwa dakika 20 na kisha nikasaini mkataba wa nyongeza. Ni rahisi sana, ninapenda sana kucheza kabumbu!β


mwakalosi
kimasihara anaweza fikia record ya rivaldo
Hamidu
Safi. Fundi wa Mpira#meridianbettz
Amani
Fundi wa mpira asiyekuwa na makuu#meridianbettz
Mwanaidi
Hahahaha anazingua huyo anasahau vipi miaka yake sasa duuh
Gabriel
Huyo mpira uko damuni ata akifika miaka 50 yuko tayar ata aende timu za wazee
Tatu
Fundi wa mpira huyo
Adelta
Namkubali Ni fundi mzuri
David pere
Bado uwezo anaa sanaa
Shafii
Inaonesha uwezo wake bado anao na anajituma sana uwanjani
Rehema Dickson
Mwenye mpira hana neno katika sekta iyo namkubal sana πͺ
Hope mwaikuka
Fresh tu
felister
bado yupo vizuriii
Ester jackson
Duuh ni hatari mpira uko kwenye damu yupo kama mm na meridian
Salma
Anazeeka na ujuzi wake
Theckla
Hilton anajua Sana mpira
Samiah
Fundi wa mpira huyo
Lydia Emmanuel Magoti
Safii sana Fundi mpira huyo
Neema juma
Bado yuko fitii sana akazane tu
Rehema
Anajua mpira sn
Ester mmakasa
Safi sana Hilton kama una uwezo wa kufanya kazi ,fanya kazi baba usiangalie umri bado unadai mbona ,na wanawake tunatakiwa kuwaunga mkono wanaume tulionao ili wajitahidi katika kutafuta kipato kama anavyofanya mke wa Hilton.
Lombo
gud newz asante
mathayo sonje
bado yuko vizuri cha msingi mazoezi ya nguvu atadumu katika soka pamoja na umri wake
aisha
sawa bwana hilton mazoezi yanakusaidia ndio maana haujui umri wako
Antony Luseno
Umri sio tatizo ki kubwa mpira bado anaucheza
Zeiyana
Safi sana hilton..!bado tunajifunza kupitia wew
Magdalena
Yupo vizuri Sana ndo maana hazeeki
Frank Patrick
Kwa league za. Wenzutu huu umri ni mkubwa sanaa kuendelea kukipiga kwenye soka
Genia Sikaluzwe
Bado yuko vizuri kwenye mpira
Neema hassan
Hilton jembee#meridianbettz
Caroline
Mpira upo kwenye damu
Kenani
Uwezo wake ndo upo juu haichuji so lazma bado ajione anasafar ndev kweny soka
Warda
Hata mie mmewangu Anamiaka 50 lakin sijawahi mkataza kucheza huko SPAIN #Meridianbettz
Juliana
Kazi na umri
Ernest
Pongezi kwako Hilton
Asha
Umri umeenda Hadi anasahau miaka yake
Sadick
Hahahahaha ni story nzuri #Meridianbettz
Povel
Duh yup vzr sana thnks meridian bet tz
Emmy cleopa
Yuko vizur
Furahav
Anatisha