Sasa ni rasmi, kocha wa zamani wa timu ya Taifa ya Italia, Roberto Mancini ndiye kocha mpya wa timu ya taifa ya Saudi Arabia na anaripotiwa kupata takriban €25m kwa msimu.
Tayari kulikuwa na ripoti kwamba mkutano na waandishi wa habari uliandaliwa kwa ajili ya hoteli siku ya leo na Shirikisho la Soka la Saudi lilitangaza kwa video jioni ya jana.
Odds kubwa kasino ya mtandaoni na michezo ya sloti ni vitu vinavyoweza kubadilisha maisha yako kwa kukupatia pesa nyingi. Ingia mchezoni hapa.
Mancini amesema; “Nina furaha kutangaza kwamba ninajiunga na Shirikisho la Soka la Saudi Arabia kama Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa. Nimefurahi na kuheshimiwa kuchaguliwa kwa jukumu hilo la kifahari, kama ishara ya shukrani na kutambuliwa kwa kazi yote iliyofanywa katika miaka hii. Napenda kumshukuru Rais Yasser Al Misehal.”
Nimekubali kukumbatia mradi mpya wa kusisimua kama huu, unaotokana na maono na madhumuni ya pamoja ya kukuza sekta ya soka ya kitaifa pamoja na vipaji vya vijana na vizazi vijavyo, ambao daima wamekuwa karibu na moyo wangu. Alisema kocha huyo.
Aliendelea kusema kuwa anaamini jukumu hilo pia ni utambuzi wa umuhimu wa mpira wa miguu wa Italia na ataendelea kuleta utamaduni wao wa Italia ulimwenguni.
Aviator, poker, Roullette, Wild Icy Fruits, Piggy Party na mingine kibao upige pesa na Meridianbet. Ingia www. meridianbet.co.tz.
Mancini alishinda EURO 2020 akiwa na Italia na kisha akashindwa kufuzu kwa Kombe la Dunia la 2022.
Alijiuzulu kutoka wadhifa wa Azzurri mnamo Agosti 13, siku tisa tu baada ya kupewa mamlaka ya ziada kama mratibu wa timu za vijana chini ya miaka 21 na 20.