Vilabu vya Mtibwa Sugar ya Morogoro na Costal Union ya Tanga vimefanikiwa kusalia katika ligi kuu ya Tanzania Bara baada ya kufanikiwa kutetea matokeo katika mechi zao za marudiano.

Coastal Union na Mtibwa Sugar zasalia rasmi VPL, Wagosi wa Kaya wakipata ushindi wa 3-1 dhidi Pamba FC ya Mwanza na kushinda kwa aggregate ya 5-3.
Mtibwa ilishinda kwa goli 4-1 katika mchezo wa kwanza dhidi ya Transit Camp na kupoteza kwa 1-0 wakiwa nyumbani lakini matokeo ya mkondo wa kwanza yanawafanya kusalia kwa 4-2.
Pamba ya Mwanza iliyopoteza playoff kwa mara ya pili mfululizo walikubali sare ya 2-2 wakiwa nyumbani kabla ya kupoteza kwa 3-1 wakiwa mkwakwani, Tanga na kuwafanya Costal kusalia kwa aggregate ya 5-3.
Je, unadhani mtindo wa kutumia playoff katika mechi za kusalia katika ligi kuu ni njia nzuri kwa vilabu vinavyotoka katika madaraja ya chini?
Kasino ya Mayan Eagle inakukufanya kuwa bingwa wakati wowote unapoamua kuicheza. Utaburudika huku ukiendelea kutengeza mkwanja mrefu, jiunge sasa na uwe miongoni mwa mabingwa!!



Sania+mapua
Vijana wamekomaa
Ernest
Mtibwa wanatakiwa kujipanga sana msimu ujao