Bondia nyota nchini Hassan Mwakinyo amesema kamwe hatishwi na rekodi za Brendon Denes wa Zimbabwe katika pambano la ubingwa wa Afrika wa ABU wa uzito wa Superwelter.
Mabondia hao watapanda uliongoni Mei 28 kwenye ukumbi wa Next Door Arena, na rekodi zikionyesha Denes HAJAPOTEZA hata pambano moja na ameshinda kwa KO katika mapambano MATANO kati ya nane aliyocheza.
Mwakinyo amesema kwa sasa anajiandaa vyema na pambano hilo na lengo lake ni kuendeleza ushindi ili kuendelea kutawala mchezo huo:
“Niko katika mfungo wa Ramadhan lakini sio kigezo cha kuacha mazoezi, bado naendelea tena kwa nguvu zaidi lengo langu ni moja tu kuwapa raha Watanzania kwa ushindi.”
Mbali na pambano hilo bondia Ibrahim Class naye atazichapa na bondia Sibusiso Zingangwe wa Afrika Kusini, wakati bondia nyota Shabani Jongo atapigana na bondia kutoka Nigeria, Olanrewaju Durodora.
TENGENEZA FAIDA KUPITIA MCHEZO WA TITAN DICE UKIWA NA MERIDIANBET KASINO
Unapokuwa kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, huna sababu ya kucheza kwa mashaka. Titan Dice, ni mchezo unaweza kukupatia mamilioni kwa mzunguko mmoja!
Venerose
Mwakinyo yupo vinzur
Sania mapua
Mwakinyo anajiamini
Johnmary jo
Nakukubali sana. Mwakinyo
Elika
Mwakinyo yuko vizuri
Mariam mtandama
Yupo vizur
Shafii
Mwakinyo yuko vizur sana kwa sasa hii kutokana na kupigana mapambano mengi makubwa.
Adelta
Kujiamini ndiyo kila kitu
Khadija
Mwakinyo yupo vzr
Issa
Tunataka ushind mwakinyo
Shakila
Yetu macho mashabiki
Saupha
Makwinyo yupo vizuri
Sauda
Mwakinyo jembe
Lydia Emmanuel Magoti
Yupo sahii
aisha
Mwakinyo mtu mbaya
neema hassan
Mwkinyo Yuko vzrii