Leo (Jana) vilabu 12 vya mpira wa miguu vimetangaza kwa pamoja kujiunga na mashindano mapya ya Super League.
AC Milan, Arsenal, Atlético, Chelsea, Barcelona, Internazionale, Juventus, Liverpool, Manchester City, Manchester United, Real Madrid na Tottenham zote zimejiunga.
Klabu zingine tatu zinatarajiwa kujiunga kama klabu za uanzishaji kabla ya msimu wa uzinduzi, ambao unatarajiwa kuanza mapema iwezekanavyo.
Katika siku za usoni, Klabu za uanzishaji zinatarajia kushauriana na UEFA na FIFA ili kufanya kazi pamoja na Super League.
Muundo wa #SuperLeague:
Mwenyekiti: Florentino Perez (Real Madrid)
Makamu mwenyekiti: Andrea Agnelli (Juventus)
Makamu mwenyekiti: Joel Glazer (Man United)
UEFA, FIFA na ligi za ndani zimetangaza kwamba watapambana dhidi ya uundwaji na kuanzishwa kwa Super League.
Msimamo rasmi wa UEFA: “Kila klabu na pia mchezaji anayeshiriki Super League anaweza kupigwa marufuku kutoka kwenye mashindano yote ya UEFA na FIFA, ngazi ya Europa au Kimataifa”.️
Msimamo rasmi wa FIFA: “FIFA imeonyesha KUKATAA kwake kwa ‘ligi ndogo za Ulaya zilzofungwa’ nje ya miundo ya mpira wa miguu ya kimataifa na bila kuheshimu kanuni”. ️
Kwa hivyo, UEFA na FIFA sasa zote zinapinga uanzishwaji wa Super League. Imekataliwa.
Nafasi nyingine kwaajili yako, kasino mpya yenye hadhi ya kipekee inayokupa kila sababu ya kuwa mshindi katika kasino za Meridianbet, anza siku yako na njia rahisi ya kutengeneza mkwanja.
Adelta
Tunasubiri kwa hamu tuone itakuwaje
Sarah
Tunasubiri tuone
warda
Mbona inapingwa sana
Lydia Emmanuel Magoti
Ngoja tuone