Beki wa kushoto wa Arsenal, Nuno Tavares atakuwa Rome kesho kufanyiwa uchunguzi wa kimatibabu Lazio, lakini gharama kamili ya uhamisho huo inatofautiana kulingana na vyanzo.

Vilabu vyote vinakubali kwamba vilipeana mikono na mchezaji huyo alikubali masharti binafsi jana, kwa hivyo ndege yake imehifadhiwa na atafanyiwa vipimo huko Roma leo.
Hata hivyo, hapa ndipo maelezo huanza kutofautiana kwa kiasi kikubwa kutoka ripoti hadi ripoti.
Sky Sport Italia inasema kuwa ni uhamisho kwa gharama ya €5m pamoja na asilimia ya ada yake ya kumuuza hapo baadae.

Mkuu wa Sportitalia Alfredo Pedullà anasema ana mkopo na analazimika kumnunua kwa jumla ya €7m pamoja na kukatwa kwa ada ya hapo baadae.
Wakati huo huo, mtaalamu Fabrizio Romano anataja takwimu hizo kama mkopo na kifungu cha lazima cha ununuzi cha €9m na tena kata ya mauzo inayofuata.
Vyovyote itakavyokuwa, Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24, atakuwa jijini Rome leo kwa uchunguzi wake wa kiafya na kutia saini mkataba wa miaka mitano.

Amerejea tu Arsenal baada ya kucheza kwa mkopo Nottingham Forest na Olympique Marseille.
The Gunners walikuwa wamemnunua Nuno Tavares kutoka Benfica kwa €8m msimu wa joto wa 2021.

